Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Namna ya Kupika Tambi za Mayai Rahisi Bila Mboga

advertisement Kupika tambi za mayai ni njia rahisi na haraka ya kuandaa mlo bila kutumia viungo vingi. Hili ni pishi linalohitaji muda mfupi na gharama ndogo, hivyo ni chaguo bora unapokuwa umechoka au una muda mfupi jikoni. Pishi hili la tambi za mayai, au “pasta” zenye mayai, linachukua takribani dakika 20 tu mpaka liko tayari kuliwa.

Mahitaji ya Kupika Tambi za Mayai

Tambi – nusu pakti (au kulingana na idadi ya watu)

Mayai – mawili au matatu

Nyanya – mbili au tatu (zilizosagwa)

Kitunguu maji – 1 (kikubwa, kilichokatwa vizuri)

Karoti – 1 (iliyokunwa)

Hoho – nusu (iliyokatwa vipande vidogo)

Mafuta ya kupikia – vijiko viwili hadi vitatu vya chakula

Sukari – vijiko vitatu vya chakula (hiari, unaweza kutumia chumvi badala yake)

Chumvi – kiasi


Maandalizi

1. Chemsha Maji: Weka sufuria jikoni na chemsha maji ya kutosha kwa ajili ya kuchemsha tambi. Wakati maji yanachemka, kata tambi zako kwa urefu unaopenda, hasa kama unatumia tambi ndefu.


2. Andaa Viungo Vingine: Saga nyanya zako vizuri, kata vitunguu kwa mtindo unaopenda, na kung’oa karoti. Kata hoho kwa vipande vidogo na weka pembeni.


3. Chemsha Tambi: Weka tambi kwenye maji yanayochemka na ongeza vijiko vitatu vya sukari (au chumvi kidogo kama unapenda). Chemsha mpaka tambi ziive vizuri. Epua tambi zako na zioshe kwa maji baridi kidogo ili zisitokane.


advertisement
4. Andaa Mchanganyiko wa Mayai: Pasua mayai kwenye bakuli, ongeza chumvi kidogo na koroga ili kuchanganya vizuri.



Hatua za Kupika Tambi

1. Kaanga Vitunguu na Karoti: Weka sufuria jikoni na ongeza mafuta ya kupikia. Ongeza vitunguu na kaanga mpaka viwe vya kahawia. Ongeza karoti na kaanga kwa dakika moja.


2. Ongeza Nyanya na Mayai: Weka nyanya zilizosagwa kwenye sufuria na pika mpaka ziive vizuri na mafuta yaanze kuonekana juu. Kisha ongeza mchanganyiko wa mayai na chumvi, koroga mpaka mayai yaive.


3. Changanya na Tambi: Baada ya mayai kuiva, ongeza tambi zilizochemshwa kwenye sufuria. Koroga vizuri ili tambi zichanganyike na viungo vingine. Mwisho, weka hoho na funika kwa dakika nne ili harufu nzuri izae na viungo vikolee.


4. Pakua na Furahia: Funua sufuria na koroga tambi zako kwa mara ya mwisho. Harufu nzuri ya tambi na mayai itajaza jikoni – ishara kuwa mlo wako uko tayari!



Jipatie Uzoefu Mpya Tambi hizi zinaweza kuliwa bila mboga ya ziada na ni chakula kamili. Kama unataka kujifunza pishi lingine la haraka, tuandikie hapo chini!


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Jinsi ya Kupika Pilau: Rahisi na Tamu

advertisement Utangulizi: Pilau ni moja ya vyakula maarufu na vinavyopendwa sana katika jamii nyingi za Afrika Mashariki. Huu ni mlo wa mchanganyiko wa mchele na viungo, ambao unaweza kuandaliwa kwa urahisi nyumbani. Katika makala hii, tutakuonyesha jinsi ya kupika pilau rahisi na yenye ladha ya kipekee. Vitu Vinavyohitajika: -2 vikombe vya mchele wa pilau -3 vijiko vya mafuta ya kupikia -1 kitunguu saumu kilichokatwa -1 kitunguu kikubwa kilichokatwa -2 nyanya za wastani, zilizokatwa -1 kijiko kidogo cha pilau masala -1 kijiko kidogo cha curry powder -½ kijiko kidogo cha cumin (caraway seeds) -3 vikombe vya maji -Chumvi na pilipili kama unavyopenda -Majani ya mviringo (bay leaves) - 2 -Karoti, ndizi za mapera (hiari) Hatua za Kupika: 1. Andaa Viungo na Mchele: advertisement Safisha mchele vizuri kwa kuusafisha na maji hadi maji yakiwa safi. Kisha, we...

Jinsi ya Kupika Ndizi Nyama za Bizari nyumbani kwa urahisi

Karibu tena jikoni! Leo tutapika ndizi nyama za bizari, chakula cha ladha nzuri na chenye virutubisho. Ndizi mbichi zinaweza kuungwa na viungo mbalimbali kama nazi na bizari ili kuongeza ladha na kuvutia mlaji. Ni mlo bora unaoweza kuwa mbadala mzuri kwa wali au ugali. Mahitaji Nyama - Nusu kilo Ndizi mbichi - Chana 3 Nazi - Nyingi (ichuje tui zito na tui jepesi) Mafuta - Nusu kikombe Pilipilimanga - Kijiko 1 Bizari ya manjano - Kijiko 1 na nusu Pilipili hoho - Kiasi Karoti - Kiasi Vitunguu maji - 2 Vitunguu saumu (thoum) - Kiasi Nyanya - 6 Tangawizi - Kiasi Chumvi - Kiasi Namna ya Kupika Ndizi Nyama Hatua kwa Hatua 1. Andaa Nyama: Katakata nyama vipande vidogo, ioshe vizuri. Kisha ongeza vitunguu saumu, tangawizi iliyosagwa na chumvi. Bandika jikoni na uichemshe hadi ianze kuiva. 2. Andaa Ndizi: Menya ndizi na uzikwangue kisha osha vizuri. 3. Andaa Viungo: Katakata nyanya, vitunguu, karoti na pilipili hoho. 4. Tengeneza Tui: Chuja tui la nazi, ambapo utakuwa na tui zito na...